Social Icons

Pages

Friday, 10 January 2014

MAPINDUZI CUP-MIAKA 50: FAINALI SIMBA v KCC!!!




   

ZANZIBAR_STONE_TOWNHUKO Zanzibar, Amaan Stadium, kwenye Mechi za Nusu Fainali, Azam FC wamenyang’anywa Taji walipotupwa nje ya Mashindano ya Mapinduzi Cup, ambalo Mwaka huu ni kusheherekea Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar, baada kuchapwa 3-2 na KCC ya Uganda iliyotinga Fainali na watakutana na Simba walioinyuka 2-0 URA ya Uganda.
Kwa Miaka miwili iliyopita, Azam FC wamekuwa Mabingwa wa Mapinduzi Cup.
Katika Mechi ya kwanza hii leo Azam FC waliongoza 2-0, kwa Bao za Chipukizi wao Joseph Kimwaga, lakini KCC wakazinduka na kuichapa Bao 3-2.
Baada ya Mechi hiyo, Simba walitinga Amaan Stadium na kubanwa na URA hadi Mapumziko kwa Bao kuwa 0-0 lakini Kipindi cha Pili Bao za Joseph Owino na Amri Kiemba ziliwapeleka Fainali.
Simba watacheza Fainali Jumatatu na KCC ambayo walikuwa nayo Kundi B kwenye Mashindano haya na kutoka 0-0 katika Mechi yao.

RATIBA/MATOKEO:
ROBO FAINALI
Jumatano Januari 8
Gombani Stadium, Pemba
KMKM 0 URA 1
Azam FC 2 Clove Stars 0
Amaan Stadium
Tusker 0 KCC 0 [KCC imesonga kwa Penati 4-3]
Simba 2 Chuoni 0
NUSU FAINALI
Ijumaa Januari 10
SAA 10 JIONI: Azam FC 2 KCC 3
SAA 2 USIKU: URA 0 Simba 2
FAINALI
Jumatatu Januari 13
Amaan Stadium
SAA 10 JIONI: Simba v KCC
 
FULU VIWANJA