
Mputu, mwenye Miaka 28 na ni Mchezaji wa Kimataifa wa Congo DR, atakuwa akilipwa Euro 40,000 kwa Mwezi.
Ingawa Mashabiki wa TP Mazembe walikuwa
hawataki Staa huyo aondoke, Klabu hiyo imetoa Taarifa kuwapoza Mashabiki
hao kuwahakikishia Klabu haitayumba kwa kuondoka kwake.
TP Mazembe inao Wachezaji wawili wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu.
Mputu amekuwa na TP Mazembe kwa zaidi ya
Miaka 10 na kuisaidia kutwaa Ubingwa wa Afrika Mwaka 2009 na 2010 na
pia kuifikisha Fainali ya Mashindano ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Klabu
Mwaka 2010 huko Abu Dhabi, Falme za Nchi za Kiarabu ambako walifungwa
Bao 3-0 na Inter Milan waliotwaa Ubingwa wa Dunia.
Januari 2012, Kabuscorp iliushangaza Ulimwengu baada ya kumsaini Gwiji wa Brazil, Rivaldo, ambae alidumu Msimu mmoja tu.