Social Icons

Pages

Thursday, 19 December 2013

MICHAEL OWEN: ARSENAL HAINA WACHEZAJI KUTWAA UBINGWA

STRAIKA wa zamani wa England, Michael Owen, amesema anaamini Arsenal inastahili kuongoza Ligi Kuu England lakini hadhani kama wana Wachezaji ambao wanaweza kumudu mbio zote hadi mwishowe kutwaa Ubingwa.
Lakini, Mchezaji huyo aliezichezea Liverpool na pia Manchester United ambayo alifanikiwa nayo kutwaa Ubingwa, amekiri kuwa Liverpool ni tofauti kwani wanao uwezo wa kutwaa Ubingwa ingawa anaamini Manchester City ndio wenye nafasi kubwa.
Ili Arsenal kutwaa Ubingwa, Michael Owen anaamini Nyota wao waliemsaini kwa Dau la Rekodi ya Klabu la Pauni Milioni 42 kutoka Real Madrid, Mesut Ozil, anapaswa kung’ara kila Mechi badala ya kuonyesha cheche Mechi moja na kisha kufifia Mechi nyingine tano.
Hadi sasa Ozil ameifungia Arsenal Bao 4 tangu atue hapo Mwezi Agosti na kusaidia kufunga Bao kadhaa lakini, Michael Owen, akiandika Ripoti yake ya Nusu Msimu kwenye Mtandao wa Sportlobster, ameeleza: “Licha ya kubamizwa hivi karibuni, Arsenal wanastahili kuongoza Ligi lakini Timu hiyo inakosa Wachezaji wenye kiwango cha kwenda mguu kwa mguu na Wapinzani wengine wanaowania Ubingwa. Licha ya Watu kuniambia mie kuwa Mesut Ozil ana kiwango cha Dunia, Mchezaji huyo hana uchezaji wa kiwango cha juu cha kudumu kila Mechi kwani tunamuona mara chache aking’ara na hufuata Mechi kadhaa akiwa amefifia!”
Owen hana wasiwasi mkubwa na Liverpool ambao amewaelezea: “Liverpool wanastahili sana kuaambiwa ni moja ya Timu inayopigania Ubingwa. Sasa wamerudi kwenye Klabu kubwa za juu. Nasikia Liverpool wanazo Fedha za kuingia Sokoni na kununua Wachezaji Dirisha la Uhamisho likifunguliwa. Ikiwa Brendan Rodgers atafanikiwa kupata lulu, siwezi kupinga wao kutwaa Taji ifikapo Mei.”HUU NDIO MSIMAMO WA LIGU KUU ENGLAND MPAKA SASA
TIMU
P
GD
PTS
1 Arsenal
16
16
35
2 Liverpool
16
21
33
3 Chelsea
16
14
33
4 Man City
16
29
32
5 Everton
16
12
31
6 Newcastle
16
-1
27
7 Tottenham
16
-6
27
8 Man United
16
6
25
9 Southampton
16
5
24
10 Swansea
16
1
20
11 Aston Villa
16
-5
19
12 Hull
16
-6
19
13 Stoke
16
-5
18
14 Norwich
16
-14
18
15 Cardiff
16
-10
17
16 West Brom
16
-5
15
17 West Ham
16
-6
14
18 Crystal Palace
16
-13
13
19 Fulham
16
-15
13
20 Sunderland
16
-18
9
 
FULU VIWANJA