Social Icons

Pages

Monday, 30 December 2013

LIVERPOOL: BRENDAN RODGERS BADO NDOTO YA UBINGWA

RAUNDI YA PILI YA LIGI: UKIONDOA MAN UNITED, VIGOGO WOTE KUTUA ANFIELD KURUDIANA NA LIVERPOOL!!
BRENDAN_RODGERSBOSI wa Liverpool Brendan Rodgers amesisitiza Timu yake bado ipo kwenye kinyang’anyiro cha Ubingwa licha ya vipigo viwili mfululizo vilivyoing’’oa kileleni na kuitupa Nafasi ya 5.
Liverpool walikuwa kileleni Siku ya Krismasi lakini sasa wapo Nafasi ya 5 Pointi 6 nyuma ya Vinara Arsenal baada kutandikwa na Manchester City na Chelsea.
Hata hivyo Brendan Rodgers bado ana matumaini na amesema: “Hamna sababu kwa nini tusigombee Ubingwa. Kitu muhimu kwetu ni kuwa bado tupo kwenye kinyang’anyiro!”
Jana Usiku Liverpool walipigwa Bao 2-1 Uwanjani Stamford Bridge na Chelsea na hii imefuatia kipigo kingine cha 2-1 Boksing Dei huko Etihad walipofungwa na Man City.
Lakini kipigo toka kwa Chelsea, ambao wako Pointi 4 mbele ya Liverpool, kimeathiri sana Kikosi cha Brendan Rodgers baada Wachezaji kadhaa kuumia kwenye Mechi hiyo.
Beki Mamadou Sakho aliumia Musuli za Pajani, Joe Allen na Jordan Henderson nao pia walipata maumivu.
Rodgers amekiri Kikosi chake ni kidogo na kina uhaba wa Wachezaji lakini wanatarajia kuimarika Mwezi Januari kwa kununua Wachezaji Dirisha la Uhamisho likifunguliwa na pia kupona kwa Nahodha wao Steven Gerrard na Straika Daniel Sturridge ambao wote walikuwa wameumia na kuzikosa Mechi kadhaa kutaongeza nguvu.
Katika Raundi ya Pili ya Ligi Kuu England inayoanza Januari Mosi, ukiwaondoa Manchester United, Timu zote za juu 8 itabidi ziende Anfield kurudiana na Liverpool na hilo limempa faraja Rodgers ambae ametamka: “Ikifika Januari tunategemea Wachezaji wote watakuwa fiti na tutaongeza nguvu Kikosini na Raundi ya Pili tutakuwa vyema. Tukibahatika kukosa majeruhi kipindi hicho, ni wazi tutapigania Ubingwa!”
 
FULU VIWANJA