Social Icons

Pages

Wednesday, 4 December 2013

JANUZAJ NAYE YUPO KWENYE LIST YA TUZO KIJANA BORA MICHEZONI

ADNAN JANUZAJ ATEULIWA KUWANIA TUZO KIJANA BORA MICHEZONI!!

MSHINDI HUPEWA TUZO YA MWANAMICHEZO BORA KIJANA KWA 2013!!
ADNAN_JANUZAJ-BOMBACHIPUKIZI kutoka Manchester United, Adnan Januzaj, amewekwa kwenye Listi ya Wagombea wa Tuzo ya BBC Young Sports Personality of the Year, ambayo hutunukiwa Kijana Bora Michezoni kwa kila Mwaka.
Waandaaji wa Tuzo hiyo ni BBC, Shirika la Utangazaji la BBC.
Januzaj, mwenye Miaka 18 na ambae Msimu huu ameanza kuichezea Timu ya Kwanza ya Mabingwa wa England, Man United, anasakwa kuzichezea Timu za Taifa za Belgium, Albania, Turkey na Serbia, ambazo ana uhalali wa kuzichezea lakini pia ataweza kuichezea England akifikisha Miaka 5 ya kuishi Nchini humo.
Listi hiyo ya Wagombea wa Tuzo ya BBC Young Sports Personality of the Year inayo Vijana 10 toka Michezo mbalimbali na itapunguzwa na kubakisha Wanamichezo watatu hapo Desemba 12 na Mshindi kutangazwa Desemba 15.
LISTI WAGOMBEA WA TUZO YA BBC YOUNG SPORTS PERSONALITY OF THE YEAR:
Dina Asher-Smith – Riadha
James Guy – Kuogelea
Amber Hill – Kulenga Shabaha
Charley Hull – Gofu
Adnan Januzaj – Football
Jessica Judd – Riadha
Amy Marren – Paralympic Kuogelea [Walemavu]
Rebekah Tiler – Kunyayua Vyuma
Isaac Towers – Riadha [Wheelchair]
Kimberley Woods – Mashua [Slalom]
 
FULU VIWANJA