Social Icons

Pages

Tuesday, 29 October 2013

YANGA WANGARA NA MBEYA CIYT YATAKATA WAMSHUSHA MNYAMA

YANGA NA MBEYA CITY ZAMSHUSHA MNYAMA .USHINDI kwa Mabingwa Watetezi Yanga na Mbeya City katika Mechi zao za leo umeishusha Simba hadi Nafasi ya 4 huku Mbeya City wakikamata Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 23 sawa na Vinara Azam FC na Yanga wakishika Nafasi ya Tatu wakiwa na Pointi 22 na Simba kuwa Nafasi ya 4 wakiwa na Pointi 20.
Timu zote hizo zimecheza Mechi 11 kila mmoja.
Huko Mjini Mbeya, ambako Timu za Mji huo zilipambana, Mbeya City iliichapa Tanzania Prisons Bao 2-0.
Jijini Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Taifa, Mabingwa Yanga waliibamiza Mgambo Shooting Bao 3-0.
Hadi Mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa Bao 1-0 kwa Bao la Dakika ya 31 la Mbuyu Twite.
Kipindi cha Pili, katika Dakika ya 50, Hamis Kiiza alifunga Bao la pili kwa Penati kufuatia Kipa wa Mgambo kumchezea faulo Didier Kavumbagu.
Bao la Tatu lilifungwa Dakika ya 67 na Didier Kavumbagu.
 
FULU VIWANJA