Social Icons

Pages

Monday, 28 October 2013

AZAM YA PETA DHIDI YA SIMBA YABEBA POINT TATU

SIMBA WALAMBISHWA DUME NA AZAM FC NA HUKO MKWAKWANI  COASTAL UNION WANGARA DHIDI YA MTIBWA SUGAR.Katika Mechi ya VPL, Ligi Kuu Vodacom, iliyochezwa leo Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, Azam FC walitoka nyuma kwa Bao moja na kuinyuka Simba Bao 2-1 na pia kuwang’oa toka kileleni na kukaa wao.
Simba walifunga Bao la katika Dakika ya 23 kwa Bao la Ramadhan Singano ‘Messi’ lakini Kipre Tchetche akaisawazshia Azam FC katika Dakika ya 43.
Katika Dakika ya 72, Kipre Tchetche tena alikwamisha Mpira wavuni na kuipa ushindi Azam FC na kuwafanya wakae kileleni wakiwa na Pointi 23 kwa Mechi 11 wakifuata Simba ambao pia wamecheza Mechi 11 na wamebaki na Pointi 20.
Huko Mkwakwani, Tanga, Wenyeji Coastal Union wameichapa Mtibwa Sugara Bao 3-0 na Bao zao kufungwa na Crispian Odula, Jerry Santo na Danny Lyanga.
Kesho Jumanne, Mabingwa Watetezi Yanga watajimwaga Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuivaa Timu ya mkiani Mgambo Shooting na ushindi kwa Yanga utawafanya wawazidi Simba kwa Pointi.LIGI HIYO ITAENDELE KESHO KWA VIWANJA VITATU KUWAKA MOTO;

Tanzania Prisons vs Mbeya City
Yanga vs Mgambo Shooting
Rhino Rangers vs JKT Ruvu
 
FULU VIWANJA